Tuesday, June 3, 2014

MAMBO YANAYOSABABISHA LUGHA KUTOKUKUA.

Kuna sababu ambazo hupelekea lugha yoyote ile kuto kukua na wakati mwingine ile lugha huweza kufa kabisa. Sababu hizo ni hizi zifuatazo:
Uhaba wa vitabu vya kufundishia, Ni sababu moja wapo ambayo hufanya lugha kuto kuendelea yani kutotumika katika elimu. Kutokana na sababu kwamba ili luhga iweze kukua inatakiwa itumike katika utolewaji wa elimu mbalimbali sasa kutokana na huu uhaba wa vitatu vya kutolea elimu inapelekea ile lugha kufa kwani inakuwa haitumiki katika masuala ya ufundishaji na vitabu kuto kutosheleza kwa kazi hiyo.

 FURAHA SANGA.

Uhaba wa Wataalamu, Lugha huweza kufa pale tu inapokosa watu muhimu wa kuindeleza. Wataalam wa lugha ndio wanaosababisha lugha kuendelea kukua na kutumika kwani wao ndio watu wa muhimu wa kusoma makala mbalimbali, vitabu mbalimbali ili tu kuendeleza lugha  husika. Kwakufanya hivyo lugha huweza  kupata misamiati mingi kutoka lugha nyingine hivyo kupelekea lugha kukua kutokana na hawa wataalam. Hivyo ni watu wa muhim katika suala zima la uenezaji wa luhga ili isiweze kufa.


Suala la Kasumba, Ni sababu ambayo hupelekea lugha kufa. Kasumba hii ni pale tu mtu anapoona lugha fulani ni bora zaidi kuliko nyingine basi ile ambayo huonekana sio bora  hufa. Watu huamini kuwa lugha ya Kiingeleza ni bora zaidi kuliko luhga ya Kiswahili na hii pia inafanya watu kuona mtu akizungumza kiingeleza  ndio msomi au anajua zaidi lugha kitu ambacho sio kweli, hivyo basi ile lugha ambayo haijathaminiwa huweza kufa.

Sera ya Lugha, Lugha ya Kiswahili hutumika kufundishia elimu ya msingi lakini sekondari na vyuo hutumika lugha ya kiingileza. Kutokana na sera ya luhga  ya nchi yetu kusababisha lugha ya kiswahili kufa kwasababu inakuwa haitumiki kwa mkazo kwani huwa kama somo tu wala sio luhga ya kutolea elimu kama ilivyo katika elimu ya msingi.

Kuwepo kwa wanyama wakali, Kuna wanyama  wakali ambao walisababisha lugha ya kiswahili kuto kukua. Mfano simba katika misitu ya tsavo kitu ambacho kilipelekea watu kuogopa kupita katika misitu hiyo na kwenda sehem nyingine kuendeleza lugha.

Makabila shupavu, Kulikuwa na makabila ambayo ni shupavu kwani hawakuruhusu misafala ya watumwa kuweza kupita katika maeneo yao. Mfano kabila la maasai wao hawakuruhusu misafala hii hivyo kusababisha lugha ya kiswahili kuto kufika katika maeneo yao.










 

9 comments: